Star wa muziki wa RnB Jason Derulo anashikiliwa na polisi baada ya kuwapiga wanaume wawili huko Las Vegas baada ya wanaume hao kumuita Usher.
Kulingana na taarifa ya polisi ni kwamba Derulo alikua anaingia katika mkahawa mmoja eneo la tukio ambapo wanaume hao wawili walimuita kwa jina la mwanamziki mwenza Usher Raymond jambo ambalo lilimkasirisha na kupelekea ugomvi huo.
Derulo alikamatwa na polisi ila wanaume hao wawili waliamua kumsamehe na kukubaliana kwamba hawatamfungulia mashtaka.