Mwanaume mmoja huko Homa Bay anashikiliwa na polisi baada ya kumkata kwa panga na kumjeruhi mamake kisa anahisi mamake hampendi vilivyo.
Kulingana na chifu wa kata ndogo ya Kwabwai Joseph Makoteng, mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 26 alimkata mamake mzazi mikono akilalamika kwamba amenyimwa mapenzi halisi ya wazazi na baadaye kutorokea msituni.
Kamanda wa polisi kaunti ndogo ua Ndhiwa Paul Rioba anasema kwa sasa mshukiwa anasubiri kufikishwa mahakamani.