Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka humu nchini Nadia Mukami amewataka mashabiki kukoma kumhukumu na maamuzi yake ya kuweka siri maisha yake binafsi.
Kupitia mtandao wake wa twitter Nadia amsema kwamba kuficha taarifa zinazohusu ujauzito wake ni maamuzi yake binafsi na hafai kamwe kuhukumiwa na mtu yoyote.
Kulingana na Nadia ni kwamba ana uhuru wa kuchagua jinsi gani anafaa kuyaishi maisha yake na hakuna mwenye haki ya kumchagulia jinsi ya kuishi.