Msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania Diamond platinum ametangaza kumrudisha tena kwenye mziki msanii wa WCB Queen Darling.
Kupitia insta story yake Diamond platinum amepachika vipande vya video vikimuonyesha queen Darleen akiwa studio akitayarisha mziki na kusema kwamba mda sasa umefika kwa mrembo huyo kurudi kwenye mziki baada ya kukaa kimya kwa mda mrefu.
Queen Darleen amekua kimya kwa kipindi cha mda mrefu kwa sasa jambo ambalo limekua likizua maswali miongoni mwa mashabiki na ujumbe huu huenda ukawa afueni kwa mashabiki.