Mwanamke mmoja huko Kaunti ya Murang’a amewashangaza wengi baada ya kuwanywesha sumu wanawe wawili na baadaye kujitoa uhai kisa mumewe anachepuka nje ya ndoa.
Akithibitisha tukio hilo naibu kamishna wa kaunti eneo hilo Anjela Makai amesema kwamba mwanamke huyo aliwaua watoto wake wawili kwa kuwanywesha sumu na baadaye kujiua kwa kujitia kitanzi.
Kulingana na ripoti yake kamishna huyo anasema mwanamke huyo aliacha ujumbe kwenye karatasi unaoeleza kwamba aliamua kujitoa uhai kisa amechoshwa na tabia ya mumewe ya uchepukaji.