Rapper toka Marekani Cardi B ameshtua wengi baada ya kusema amechoka kuwa maarufu.
“Kuwa staa kunachosha”
Cardi B amesema haya kupitia akaunti yake ya mtandao wa Twitter, bila ya kueleza zaidi sababu msingi iliyopelekea kuandika ujumbe huo.
Kauli hiyo imepokelewa na hisia tofauti huku wengine wakimuunga mkono wakisema kuwa staa kunafanya maisha yako yakose usiri, ilhali wengine wakimpinga na kuhoji kuwa maarufu huleta pesa na kwamba kuwa masikini kunachosha zaidi kuliko kuwa maarufu.