Dj mkongwe nchini Dj Pinye amezua gumzo baada ya kusema kwamba aina ya mziki maarufu wa Gengetone hauwezi vuka mipaka.
Pinye anasema mashairi na mtindo wa mziki huo hauna mpangilio na ubora wake haufikii viwango vya kufanya vizuri kwenye soko la kimataifa.
Aidha Pinye anasema wasanii wa mziki wa Gengetone wametosheka na soko la Kenya na hawajajipatia changamoto ya kutayarisha mziki kwa ajili ya soko la kimataifa.