Msanii wa mziki wa kizazi kipya mbaye pia ni mbunge wa starehe kaunti ya Nairobi Jaguar amewaomba wasanii kukoma kumtafuta wakati wako na shida za kifedha.
Jaguar anasema alichaguliwa kama mwakilishi wa wakaazi wa eneo bunge la starehe na kazi yake kuu kama mbunge ni kuwahudumia wakazi wa eneo bunge hilo pekee.
Kulingana na Jaguar ni kwamba kuna fikra potofu miongoni mwa wasanii kwamba ana jukumu la kuwasaidia wasanii nchini sababu aliwahi kuwa msanii miaka ya nyuma.