Msanii Wizkid kutoka Nigeria amewahakikishia mashabiki kwamba yeye na wasanii mwenza Burnaboy pamoja na Davido, hawajawahi kuwa na tofauti zozote kati yao.
Wizkid amesema kwamba watatu hao ni marafiki wakubwa na wanapendana saana.
Kulingana na Wizkid ni kwamba watatu hao wanapambana kwa Pamoja sio tu kuupeleka mziki wa nchi hiyo mbele bali pia katika kusaidiana kufanikisha malengo ya kila mmoja wao.
Matamshi haya ya Wizkid yanajiri siku chache tu baada ya kuonekana pamoja na Davido wakikumbatiana licha ya kusemekana kwamba wawili hao wana tofauti