Msanii Willy Paul ametangaza kuwasamehe watu wote ambao walimsababishia maumivu hasa kwenye safari yake ya mziki.
Willy Paul anasema ameamua kuwasamehe adui zake baada ya kupona kutokana na msongo wa mawazo ambao ulikua ukimuandama.
Kulingana na Willy Paul ni kwamba tangu alipoamua kuwasamehe maadui zake mungu amekua akimfungulia milango ya mafanikio kwenye mziki Pamoja na biashara zake.