Producer Nguli wa mziki kutoka Nigeria Don Jazzy ameelezea kusikitishwa kwake na taarifa za ujauzito wa star wa mziki kutoka marekani Rihanna.
Kupitia mitandao yake ya kijamii Don Jazzy ameelezea kusikitishwa kwake na taarifa hizo na kudai kwamba mbio zake za kumtaka mrembo huyo hatimaye zimegonga mwamba.
Kulingana na Don Jazzy ni kwamba ndoto yake ya kumpata mrembo huyo kwa sasa zimeingizwa doa na ujauzito huo na kwa sasa hana budi kukata tamaa.