Star wa mziki kutoka Marekani Rihanna pamoja na mpenzi wake Rapper ASAP Rocky wametangaza rasmi kwamba wanatarajia mtoto.
Kupitia picha ambazo wameziachilia kwenye mitandao wawili hao wametangaza ujauzito huo na kuuweka wazi kwa mashabiki wao kwamba hivi karibuni wanatarajia kupata mtoto.
Picha hizo za ujauzito ambazo kwa sasa zinasambaa kwenye mitandao mbali mbali zilipigwa jijini New York wikendi iliyopita.