Lejendari wa mziki wa Genge kutoka Nairobi Jua Cali amesema kwamba hakuna cartels kwenye kiwanda cha mziki kama wengi wanavyofikiria bali ni fikra potofu tu ambayo wasanii wamejiwekea.
Jua Cali anasema fikra kwamba kuna kikundi cha watu kinachoamua msanii gani anafanya vyema katika soko la mziki ni uongo na mawazo potofu.
Msanii Jua Cali amewashauri wasanii kuwacha kulalamika.
Msanii Shata wale kutoka nchini Ghana amezua gumzo baada ya kuwajia juu wasanii wanaodai anaiga mtindo wa mziki kutoka taifa jirani la Nigeria.
Kupitia mtandao wake wa twitter shatta wale amesema kwamba inashangaza kuona kwamba malalamishi hayo yanatoka kwa washikadau wa mziki pamoja na wasanii ambao anawaheshimu.