Familia ya nguli wa mziki wa Reggae Bob Marley wamefungua rasmi maonyesho ya gwiji huyu huko jijini London nchini uingereza.
Maonyesho hayo ambayo yamepewa jina la One Love experience yanatarajiwa kufanyika kwa mda wa takriban siku kumi kuenzi Maisha ya Bob Marley.
Kulingana na waandalizi wa maonyesho hayo ni kwamba wanalenga kuonyehsa mashabiki wa msanii huyo baadhi ya vitu alivyovitumia Pamoja na picha mbali mbali zitakazoonyesha Maisha halisi aliyowahi kuishi Bob Marley.