Msanii Otile Brown anamtaka mpenzi wake wa zamani Vera Sidika kukoma kumtataja mara kwa mara katika mahojiano, baada ya Vera Sidika kunukuliwa akiweka wazi kwamba yuko tayari kusimamia collabo baina ya mpenzi wake Brown Mauzo na msanii Otile Brown.
Otile Brown anasema tabia ya mrembo huyo kumtaja taja mara kwa mara katika mahojiano na vyombo vya habari ni kumkosea heshima mumewe wa sasa Brown Mauzo.
Otile Brown amesistiza kwamba anaheshimu mahusiano mapya ya mrembo huyo na msanii Brown Mauzo na ndio maana hua anajaribu sana kujiweka mbali naye lakini haelewi kwani Vera Sidika anamchokoza mara kwa mara.