Watafiti wa kisayansi kutoka Ujerumani wameanzisha ufugaji wa ngurue maalum kwa ajili ya kuvuna mioyo yao, itakayotumika kupandikizwa kwa binadamu nchini Marekani.
Kulingana na Eckhard Wolf mwanasayansi kutoka jiji la Munich nchini Ujerumani, yeye na wanasayansi wenzake wako mbioni kwa sasa kuchangaya mbegu tofauti za aina mbali mbali za nguruwe ili kupata aina maalum ambayo mioyo yao itatumika kupandikizwa kwa binadamu wenye matatizo.
Wazo hili linajiri mwezi mmoja tu baada ya madaktari chuo kikuu cha Maryland huko nchini marekani kufanikiwa kupandikiza moyo wa ngurue kwa binadamu.