Msanii Kanye West kutoka nchini Marekani ameelezea kughadhabishwa kwake na hatua ya binti yake mwenye umri wa umri wa miaka 8, kuwepo kwenye mtandao wa kijamii wa Tik Tok.
Kanye ameelezea hasira zake baada ya kugundua kwamba mwanawe North West ana akaunti ya Tiko Tok, bila idhini yake kama baba mzazi.
Kulingana na Kanye ni kwamba anahitaji majibu kutoka kwa mzazi mwenza Kim Kardashian kuhusu swala hilo maana ana haki ya maamuzi kama baba kwa maisha ya watoto wake.