Mwanamke mmoja kutoka jimbo la Ogun huko Nigeria anashikiliwa na polisi baada ya kumuua binamu ya mumewe kisa amevunja kioo cha kujipambia.
Cynthya Olukiowu mwenye umri wa miaka 30 alimuua kwa kumdunga kisu binamu ya mumewe baada ya wawili hao kugombania kioo.
Kulingana na taarifa ya polisi ni kwamba mshukiwa alipandwa na hasira na kumdunga kisu Habeeb Aremu mwenye umri wa miaka 18 na kumuua papo hapo.