Rapper Drake amezua gumzo mitandaoni baada ya kumzawadia shabiki mmoja dola 10,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni moja pesa ya Kenya kama zawadi ya Birthday yake.
Rapper huyo ambaye alikua kwenye likizo kwenye visiwa vya Turks and Caicos vilivyoko bahari ya Atlantic aligundua kwamba mmoja kati ya mashabiki wake alikua eneo alilokua akijivinjari akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na alinyanyuka na kwenda kwake moja kwa moja na kumpa zawadi ya pesa hizo.
Drake ni mmoja kati ya rappers ambao wanajulikana kwa kutoa misaada na zawadi ikikumbukwa kwamba kuna mda aliwahi kutumia pesa alizokua amezipangia kwa utayarishaji wa video ya wimbo wake mmoja na kuwasaidia watu katika jimbo la Miami nchini Marekani.