Msanii Davido kutoka nchini Nigeria ameonyesha kukerwa na uvumi uliokithiri mitandaoni kwamba yeye sio baba halisi wa mmoja kati ya watoto wake.
Kupitia mtandao wake wa twitter Davido amesema kwamba hatakubali kamwe watu kuichafulia jina familia yake na madai ambayo hayana msingi.
Davido ametishia kumchukulia hatua za kisheria mtu yoyote ambaye atasambaza madai yoyote ya uongo kuihusu familia yake.