Mwanamtindo maarufu nchini Marekani Kylie Jenner na mumewe Travis Scott wametangaza kubadili jina la mtoto wao waliyezaa wiki sita zilizopita.
Mtoto huyo wa kiume alikua amepewa jina la Wolf Jacques Webster alipozaliwa tarehe 6 Februari mwaka huu, lakini sasa wazazi wake Kylie na Travis wanata kuliondoa jina la “Wolf” kutoka katika majina yake rasmi, katika hati yake ya kuzaliwa.
Akitangaza hatua hiyo, Jenner amesema wao kama wazazi wamekubalana kwamba jina “Wolf” halimfai mtoto wao na kufichua kuwa tayari wameweka ombi rasmi kwa afisi ya usajili wa majina na Watoto nchini Marekani wakingoja ombi lao la kubadili jina la mtoto wao kukubaliwa rasmi.