Msanii Otile Brown amezua gumzo mitandaoni baada ya kujinunulia zawadi ya viatu vyenye thamani ya shilingi 80,000 madukani.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Otile Brown ameonyesha viatu hivyo aina ya Balenciaga na kusema kwamba ni zawadi yake ya siku yake ya kuzaliwa.
Otile Brown aidha anasema uwezo wake wa kununua viatu aina hio ni inshara tosha kwamba anajiweza kifedha na ako tayari kushindana na wasanii wengine kifedha na mziki.