Msanii wa hip hop kutoka nchini Tanzania Roma anasema wasanii wengi wenye kipaji cha kuimba wanasumbuliwa na uvivu katika tasnia ya mziki.
Kupitia mtandao wake wa twitter Roma amesema kwamba tasnia ya mziki kwa sasa imetawaliwa na wasanii wengi wenye kiwango cha chini cha kipaji lakini wenye bidii.
Roma ameeleza kuwa wasanii wenye vipaji wameshindwa kimziki na wasani ambao hawana vipaji lakini wanajituma zaidi.