Vita vya mitandaoni miongoni mwa ma Star kutoka Nigeria na Ghana vimezuka baada ya Ghana kuwabandua Nigeria kushiriki kwa michuano ya kombe la Dunia.
Baada tu ya mechi ya jana ma star kutoka Ghana wakiongozwa na mwanamziki Shata Wale walivamia mitandao ya kijamii na kuwakejeli wa Nigeria kwa kuwaita Super Chickens badala ya Super Eagles baada tu ya mechi ya jana.
Mechi hiyo ya jana inaonekana kuongeza uhasama wa kimichezo na Sanaa uliopo kati ya nchi hizo mbili zinazopakana huku mashabiki wa Nigeria wakisababisha uharibifu mkubwa uwanjani kufuatia hasira za kupoteza mechi hiyo.