Msanii Burna Boy kutoka nchini Nigeria anasema wimbo wake kwa jina ‘Last Last’ kutoka kwa album yake ya punde zaidi ‘Love, Damini’ ndio wimbo uliomtilia fedha nyingi zaidi katika historia ya sfari yake ya mziki.
Burna Boy amefichua haya katika mahojiano ambapo ameeleza kuwa, kinyume na wengi wanavyodhani, mgao wake wa asilimia 40% katika makubaliano yake na Toni Braxton katika wimbo huo bado unapatia hela nyingi.
Wimbo ‘Last Last’ ni miongoni mwa nyimbo 19 katika album ‘Love, Damini’ na tayari ameupangia kuufanyia remix na msanii Dave ambaye ni rapper anayeishi Uingereza mwenye asili ya Nigeria.