Wanasayansi wanasema jumatatu ya juzi tarehe 29 mwezi wa Julai ndio siku fupi zaidi kuwahi kurekodiwa duniani baada ya kutofikisha masaa 24 kama kawaida ilivyozoeleka.
Kulingana na ripoti ya wanasayansi, siku ya jumatatu dunia ilizunguka kwa uharaka zaidi na kufanya siku hiyo kuwa fupi na sekunde 1.59.
Wanasayansi wanasema hii ni tofauti na mtindo ambapo siku zimekua zikiwa ndefu zaidi hadi kufikia masaa 24 kwa sasa kadri miaka inavyosonga.
Wanasayansi wameeleza kuwa zamani kama miaka bilioni 1.4 iliyopita, siku moja duniani ilikua ikichukua masaa 19 pekee tu.