Wanasayansi wamefanikiwa kufufua viuongo vya mwili wa nguruwe, jisaa moja baadae baada ya nguruwe kufariki.
Kwa kawaida mnyama anapofariki huanza kuoza pindi damu inaposita kusambaa katika viungo, baada ya moyo kusimama na kwa mda imekua hakuna njia ya kuamsha/kufufua tena viungo vya mwili wake.
Katika uvumbuzi uliochapishwa katika jarida la wanasayansi la Nature, wanasayansi wameeleza kuwa walipitisha damu ya kujitengenezea katika maabara katika mishipa ya damu ya nguruwe aliyefariki jisaa moja baade na damu waliyotengeneza ilifanikiwa kufufua uhai wa baadhi ya viungo vya ndani vya nguruwe aliyefariki na kuvirudisha katika ubora wa uhai wake.
Wanasayansi wameeleza japo walishindwa kufufua kiungo cha ubongo, uvumbuzi huu umeibua matumaini katika ulimwengu wa matibabu, kuhusu kufufua binadamu anapofariki.