Hatimaye ma’producer wakongwe ulimwenguni P Diddy na Dr. Dre wameamua kufanya kazi ya kwanza kwa pamoja katika historia yao ya safari ya mziki.
Kulingana na taarifa nchini Marekani, P diddy amefika kwa Dr. Dre kufunzwa vitu flani kuhusu mziki, ikiwemo matamshi ya maneno katika nyimbo.
Picha inayowaonyesha wawili hao wakiwa studio imesambaa kwa kasi mitandaoni na kuzua hisia mseto kuhusu kazi ya pamoja itakayozaliwa kutoka na ushirikiano wao.
Imeelezwa kuwa nguli hawa wa mziki hip hop duniani, wameingia studio kutengeneza wimbo wa pamoja kusaidia kampeini mpya ya P Diddy inayokwenda kwa jina la “R&B is Dead.”