Watu watatu wamefariki katika ajali ya ndege jimbo la Colorado nchini Marekani, katika kisa ambapo ndege mbili ziligongana zikiwa hewani kabla ya kuanguka.
Kulingana na ripoti ya polisi wa mji wa Boluder zilikoanguka ndege husika, ndege aina ya Cessna 172 iligongana na ndege aina ya Sonex Xenos hewani huku kiini cha ajali ikiwa bado hakijabainaka.
Ajali hiyo imetokea karibu na uwanja wa ndege wa Vance Brand Airport.