Madaktari nchini Italia wamefichua tukio la upasuaji wa ubongo ambapo mgonjwa aliyekua akifanyiwa upasuaji wa kichwa alilazimika kupiga tarumbeta huku akiendela kufanyiwa upasuaji na madaktari.
Paideia International Hospital katika mji wa Rome imefichua kuwa mgonjwa mmoja mwenye umri wa miaka 35, alipiga tarumbeta mda wote wa masaa tisa akifanyiwa upasuaji wa kutoa uvimbe katika ubongo wake, ili kuwapa uwezo madaktari kutathmini uwezo wa sehemu tofauti za ubongo wake wakiufanyia upasuaji.
Madaktari wameeleza upigaji tarumbeta uliwawezesha kutathimni uwezo wa mgonjwa kucheza, kuzungumza,kukumbuka vitu na hat kuhesabu vita wakati upasuaji ukiendelea