Jamaa mmoja raia wa Marekani amezua gumzo mitandaoni baada ya kufanikiwa kula kuku mzima kila siku kwa kipindi cha siku 40 mfululizo.
Alexander Tominsky, kutoka jimbo la Philadelphia mwenye umri wa miaka 31 amekua akipeperusha ulaji wake wa kila kuku mzima kwa siku hizo 40 katika mtandao wa twitter.
Tominsky amekua akizua gumzo katika mtandao wa twitter kila wakati anapokwenda LIVE akila kuku mzima hadi kupewa jina la kimajazi la ‘Philadelphia Chicken Man’.