Jamaa mmoja amengia katika vitabu vya kumbukumbu za rekodi za dunia baada ya kufanikiwa kujaza vibofu 28 kwa kutumia pua kwa kutumia kipindi kifupi zaidi duniani.
David Rush kutoka jimbo la Idaho nchini Marekani amefanikiwa kuvijaza vibofu hivyo kwa mda mchache zaidi kuwahi rekodiwa duniani, ambao ni dakika 3.
Rush ambaye pia anashikilia rekodi zengine za kufanya vitu tofauti duniani, anasema amejaribu kuweka rekodi hiyo ya kujaza vibofu mara 42 kabla ya hatimaye kufanikiwa majuzi.