Inaripotiwa msanii The Weeknd alilazimika kusitisha katikati kutumbuiza katika tamasha lake wikendi hii, baada ya kupoteza sauti yake ghafla.
Kulingana na taarifa nchini Marekani, The Weeknd aliimba wimbo mmoja kabla ya kwenda backstage kujitayarisha kwa wimbo wa pili, lakini wakati ulipofika kuimba wimbo wa pili sauti ilipotea kabisa na kuchanganya mpagilio wa kutumbuiza.
Inasemakana ukumbi ulikua na watu 70,000 ndani tayari na alikua ametumbuiza kwa dakika 15 tu kabla ya kupoteza sauti.