Raia mmoja wa taifa la Uingereza ameweka rekodi mpya katika vitabu vya kumbukumbu duniani, baada ya kufanikiwa kunywa pombe katika mikahawa (bar) 67 tofauti katika mda wa masaa 24.
Nathan Crimp, mwenye umri wa miaka 22, alifanikiwa kuingia “bar” hizo 67 katika mji wa Brighton katika mda wa masaa 17.
Crimp alikua ameandamana na marafiki, wakilenga kuvunja rekodi ya awali ya “bar” 56 ililiyokua imewekwa na jamaa mmoja kwa jina Gareth Murphy katika mji wa cardif mapema mwaka huu.