Mashabiki wamejitokeza kumchangia msanii Kanye West ili arudie hadhi yake ya kuwa bilionea ulimwenguni, baada ya kampuni kadhaa kukatiza uhusiano wa kibiashara na yeye kufuatia matamshi yake ya kiubaguzi dhiidi ya watu wenye asili ya kiyahudi.
Kupitia mtandao wa GoFundMe, mashabiki hao wanataka kumuongezea fedha Kanye West baada ya kuteremka katika orodha ya matajiri duniani kufuatia hatua ya biashara zake kadhaa kukatizwa.Akikiriri kupungua kwa utajiri wake ghafla, Kanye West amefichua kuwa kuna siku alipoteza utajiri wa bilioni mbili baada ya kampuni ya Adidas kujiunga na kampuni kadhaa zilizoamua kukatiza uhusiano wa kibiashara naye.