Chuo moja kikuu nchini Ufaransa kimezua gumzo baada ya kutangaza kuanzishwa kwa masomo ya master’s degree katika mafunzo ya unywaji pombe, ulaji chakula na jinsi ya kuishi maisha mazuri.
Chuo cha Sciences Po kutoka mji wa Lille nchini Ufaransa, kimesajili wanafunzi 15 ambao watafunzwa jinsi ya kula vizuri, kunywa pombe vizuri, pamoja na kuishi maisha mazuri yar aha mstarehe.
Kupitia masomo mbali mbali ya ulaji vyakula tofauti vya binadamu, wanafunzi watakaokamilisha masomo hayo watapewa cheti cha uzamili (master’s degree) katika swala la kula, kunywa na kuishi vizuri maisha.