Msanii wa mziki wa kizazi kipya ambaye pia ni mwanasiasa kutoka Uganda Bobi Wine amezua gumzo nchini Uganda baada ya kutoa wimbo unaomponda raisi wa taifa hilo Yoweri Museveni.
Wimbo huo umezungumzia maovu ambayo kulingana na Bobi Wine yamefanywa na utawala wa Museveni.
Bobi Wine pia ameelezea kusikitishwa kwake na umoja wa mataifa kukaa kimya wakati waganda wanateseka chini ya utawala m’baya.