Gumzo limezuka mitandaoni baada ya mwanamke mmoja anayedai kuwa baby mama wa msanii wa Konde Gang Ibra kudai kujitokeza na kudai msanii huyo hawajibiki majukuma yake kama baba.
Mrembo huyo kwa jina Kim Mishepu amedai kwamba tangu ajifungue mtoto huyo hajawahi kabisa kupata msaada kutoka kwa msanii huyo na kwamba alimlazimisha aweke kila kitu siri ili kuilinda brand yake.
Kulingana na mrembo huyo ni kwamba kilichomsukuma kuweka kila kitu wazi ni kwa sababu ya mateso anayopitia bila kupata msaada wowote.