Member wa kundi la mziki la Sauti Sol kwa jina Polycarp Fancy Fingers amewashtumu wasanii wanaojitosa kwenye siasa, akiwataja kama wasiokua na wito wowote wa uongozi bali ubinafsi.
Polycarp anasema inasikitisha kuona wasanii wengi wanadanganyika na umaarufu walionao kwenye Sanaa wakidhani kwamba utawapa mafanikio ya moja kwa moja kwenye ulingo wa siasa.
Kulingana na Polycarp ni kwamba wasanii wengi wanaojiingiza kwenye uongozi hawana wito wowote wa kumpigania mwanainchi bali wanaingia tu kutafta maslahi yao binafsi.