Msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Uganda Cindy amezua gumzo baada ya kusema kwamba atayauza magari yake na kugeukia usafiri wa baiskeli.
Kupitia mitandao yake ya kijamii msanii huyo amekiri kwamba ugumu wa maisha pamoja na kupanda kwa bei ya mafuta nchini humo kumempelekea kuamini kwamba magari yanamsababishia hasara tupu katika maisha na mipango yake ya muziki.
Kauli hii ya Cindy inajiri wakati ambao wanainchi wamekua wakiishinikiza serikali kufanya jitihada ya kuhakikisha inadhibiti bei ya mafuta nchini humo.