Msanii Jose Chameleone kutoka Uganda anataka washikadau wa mziki nchini Uganda kutambua mchango wake katika mziki wa taifa hilo akiwa bado yungali hai na kutosubiri hadi afariki kumuenzi.
Chameleone anasema inasikitisha kuona kwamba mchango wa wasanii wengi hautambuliki licha ya kwamba wanahangaika na kuupigania mziki wa taifa hilo kuvuma kimataifa.
Akitoa mfano wa wasanii Mozey na Radio, Chameleone amesema inasikitisha kwamba washikadau wengi wa mziki nchini Ugandaq hawatambui juhudi za wasanii hadi pale wanapoaga dunia.