Rapper kutoka Nairobi Femi One amezua gumzo mitandaoni, baada ya kuelezea matamanio yake ya kuolewa na mwanamuziki Patoranking kutoka Nigeria.
Kupitia kujibu maswali kutoka kwa mashabiki wake katika ukurasa wake wa Instagram Femi One ameweka wazi matamanio yake ya kuolewa na msanii Patoranking, wakati akimjibu mmoja wa mashabiki wake aliyemuuliza kuhusu mipango yake ya kuolewa.
Kulingana na Femi One ni kwamba upendo wake kwa Patoranking hauelezeki na kufikia sasa kwenye fikra zake tayari yuko kwenye ndoa na msanii huyo kutoka Nigeria licha ya kwamba hajui.