Msanii toka Tanzania Diamond Platnumz ameweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye show maalum iliyoandaliwa na waandaaji wa tuzo za Grammy inayokwenda kwa jina la GlobalSpin
Show hii ambayo inaruka kwa njia ya mtandao kupitia akaunti za YouTube, Twitter, Facebook za Grammy Academy ilianzishwa mwaka 2021 kwa lengo la kuutangaza zaidi muziki wa afrika na wa kilatino.
Diamond Platnumz ameimba wimbo wake mpya ambao haujawahi kutoka kwa jina #Gidi.