Msanii wa nyimbo za injili Mercy Masika ametoa wito kwa wanawake walioko kwenye kwenye ndoa kuwaheshimu waume zao.
Mercy amesema kwamba wanaume wanahitaji kuzungumziwa kwa heshima inayostahili ili kuitunza ndoa.
Kulingana na Mercy ni kwamba ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya wanawake kuwa na kiburi cha kupitiliza kwa waume zao.