Msanii Davido wa Nigeria ametaja kudra za mwenyezi mungu kama sababu kuu iliyopelekea kufanikiwa kwake kuujaza ukumbi wa 02 arena jijini London wikendi iliyopita katika tamasha lake.
Kupitia akaunti yake ya instagram Davido amesema kwamba mbali na uwezo wake kwenye mziki ilikua muujiza mkubwa kwa tiketi za tamasha hilo kuisha zote kinyume na alivyotarajia.
Kulingana na Davido ni kwamba tamasha hilo lilikumbwa na changamoto nyingi na kufanikiwa kwake haikuwa nguvu za mwanadamu.