Star wa muziki kutoka Nigeria Davido amezua gumzo baada ya kununua gari lengine lenye thamani ya takriban naira milioni 90 ambazo ni sawia na milioni 24.6 pesa za Kenya.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Davido ameonesha gari hilo aina ya Mercedes Benz Maybach SUV masaa machache tu baada ya tamasha lake alilolifanya katika ukumbi wa 02 Arena jijini London.
Mkoko huu ni mmoja kati ya magari ya gharama ambayo star huyu anayamiliki.