Star wa mziki kutoka Nigeria Burna Boy anaandamwa na kashfa mpya baada ya mwanamke mmoja kutangaza kwamba hajamlipa pesa ya chakula alichomuuzia.
Kulingana na mwanamke mmoja kwenye mtandao Instagram anayejitambulisha kwa jina la kibiashara Bone And Fish ni kwamba Burna Boy alitangaza mitandaoni kwamba atamlipa mtu yoyote ambaye atamtayarishia chakula hicho maalum pauni 10,000 ambazo ni sawia na milioni moja na nusu pesa ya Kenya.
Hata hivyo baada ya kutayarisha na kuwatumia chakula hicho hadi sasa Star huyo Pamoja na usimamizi wake haujamlipa pesa yake.