Watu 4 wamenaswa na polisi nchini Marekani baada ya kutumia kifaa maalum kupunguza bei ya mafuta katika vituo vya uuzaji mafuta ya gari, ili wananchi wanunue mafuta kwa bei ya chini.
Kifaa hicho maarufu kwa jina ‘pulsators’ kina uwezo wa kubadli bei katika mashini za kujaza mafuta bila ya wahudumu kujua.
Wanne hao wanatuhumiwa kutekeleza uhalifu huo katika jimbo la Florida wakati ambapo dunia inashuhudiwa kupanda kwa bei zamafuta na idara ya polisi nchini Marekan inasema watafikishwa mahakamani kujibu mashataka ya wizi.