Jamaa wawili raia wa Italia wamengia katika vitabu vya rekodi za dunia baada ya kufanikiwa kubadilisha tairi la gari wakati gari likiwa linaenda kwa kasi.
Manuel Zoldan na Gianluca Folco walifanikiwa kubadili tairi ya gari lao aina ya BMW 3-Series likiwa linaenda kwa muda wa dakika moja na sekunde 17.
Kulingana na wawekaji rekodi za dunia, wawili hao wamevunja rekodi ya awali ambayo ilikua ni dakika moja na sekunde 30.