Utafiti mpya umebaini kwamba ulaji ndizi unapelekea kuimarika kwa hali ya afya ya moyo wa binadamu.
Kulingana na utafiti uliofanywa na Dr. Liffert Vogt kutoka chuo kikuu cha Amsterdam nchini Uholanzi, ndizi imesheheni madini mengi ya potassium ambayo hubadili uharibifu unaoletwa na ulaji chumvi nyingi katika mwili wa binadamu.
Dr. Liffert ameeleza kuwa ulaji chumvi nyingi husababisha shinikizo la damu, lakini mtu anapokula ndizi, madini ya potassium husaidia kusafisha chumvi na kuimarisha moyo wa binadamu.